GEITA; SERIKALI kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imeanza kutekeleza mradi wa huduma ya intaneti ya bure kwenye maeneo ya wazi ikiwemo masoko na vituo vya afya mkoani Geita. Mkuu wa UCSAF Kanda ya Ziwa, Fredy Kandonga alieleza hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya mawasiliano Mkoa wa Geita mbele ya Kamati …