WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amesema maendeleo ya kudumu ya Taifa hayawezi kupatikana bila kujenga wananchi wenye maadili, uzalendo, uwajibikaji na mshikamano, sambamba na kuendelea kuimarisha utawala wa sheria na taasisi za umma.